SEHEMU YA 74
Baada ya Joseph Smith, Mdogo, kuanzisha upya masahihisho ya Maandiko yaliyovuviwa, “alipokea maelezo yafuatayo ya Waraka wa Kwanza kwa Wakorintho, sura ya 7, mstari wa 14.”
1 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama sivyo, watoto wenu wangekuwa najisi; lakini sasa wao ni watakatifu.
2 Sasa katika siku za mitume sheria ya tohara ilikuwapo miongoni mwa Wayahudi wote ambao hawakuiamini Habari Njema ya Yesu Kristo.
2b Na ikawa kwamba kulitokea mabishano makubwa miongoni mwa watu kuhusu sheria ya tohara, kwani mume asiyeamini alitamani kwamba watoto wake watahiriwe na kuwa chini ya Sheria ya Musa, ambayo sheria ilitimizwa.
3a Na ikawa kwamba watoto wakilelewa chini ya Sheria ya Musa, na kutii mapokeo ya baba zao, hawakuamini injili ya Kristo, ambayo kwayo hawakuwa watakatifu;
3b kwa sababu hiyo mtume aliandikia kanisa, akiwapa amri, si kutoka kwa Bwana, bali kwatoka kwake yeye mwenyewe, kwamba mwamini asiunganishwe na mtu asiyeamini, isipokuwa Sheria ya Musa ikatishwe kati yao, ili watoto wao wakae bila kutahiriwa;
3c na ili mapokeo yaondolewe, ambayo yanasema kwamba watoto wadogo si watakatifu, kwani ilikuwa miongoni mwa Wayahudi;
3d lakini watoto wadogo ni watakatifu, wametakaswa kwa njia ya upatanisho wa Yesu Kristo; na hivi ndivyo Maandiko yanamaanisha.
Maktaba ya Maandiko: Mafundisho na Maagano
Kidokezo cha Utafutaji
Andika neno moja au tumia manukuu kutafuta kifungu kizima (km "kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu").
Kwa rasilimali za ziada, tafadhali tembelea yetu Rasilimali za Wanachama ukurasa.